Tuesday, September 11, 2007

TAMWA- mmeyasikia haya?

Ni siku ya pili tangu mkutano mkubwa unaojulikana kama Highway Africa Conference 2007 uanze hapa Grahamstown, ambapo katika kipindi cha pili wanamama mashujaa walipangua mada za washiriki ambao walitaka kujua nini haswa maana ya Gender.

Kwa kweli kama ungekuwepo kwenye ukumbi wa Eden Grove Red, usingesita kuwaita mashujaa kwa jinsi walivyoweza kuzijadili haswa hoja za wanaharakati mbalimbali ambao kwa mlengo wangu naona walikuwa ama hawaoni umuhimu wa kuwa sera za jinsia kwenye taasisi za habari.

Kristin Palitza- huyu ni mwenyekiti wa GEMSA - hii ni taasisi ya masuala ya jenda ambaye ALITOA OVERVIEW ya Professionalism in the Newsroom; the gender Dimension.
Ama kwa hakika huyu mama ameshiba katika eneo hilo lakini maswali ya wasikilizaji yaliniacha hoi kwani, nawanukuu "wanaowagandamiza wanawake ni wanawake wenyewe..."

Wanawake ni walezi wa watoto kwanini hawaoni ulazima wa kuwafundisha watoto atittude za kuwa gender sensitive tangu wakiwa wadogo? Wanawake hao hao ndio chanzo kikubwa cha maendeleo yao wenyewe, chukua mfano inapofikia uchaguzi wa nchi or whereve... haya what is gender and sex? kwanini kama wanawake wanazungumzia maswala ya gender, mbona hakuna mwanaume kwenye panel ya watoa mada kuonyesha usawa, hahahaaaaaaaaaa.

Ni hayo tu kwa sasa

3 comments:

kifimbocheza said...

karibu sana dada

Ansbert Ngurumo said...

Karibu sana kwenye dunia ya wanablogu. Jifunze kwa waliokutangulia; nawe wafunze unayojua.

Ansbert Ngurumo said...

Karibu